Tuesday, April 1, 2014

DURBAN, EDMONTON ZATUMA RASMI MAOMBI YA KUANDAA JUMUIYA YA MADOLA 2022.

MIJI ya Durban na Edmonton amethibitisha rasmi nia yao ya kuandaa michuano ya 22 ya Jumuiya ya Madola mwaka 2022. Afrika Kusini haijawahi kuandaa michuano hiyo toka ianzishwe, wakati Mji wa Edmonton uliopo nchini Canada wenyewe waliwahi kuandaa mwaka 1978. Rais wa Shirikisho la Michuano ya Jumuiya ya Madola-CGF, Tunku Imran amesema nia iliyoonyeshwa na miji hiyo ni dalili chanya za kukua kwa michuano hiyo. Michuano ya 20 ya Jumuiya ya Madola inatarajiwa kufanyika jijini Glasgow Julai mwaka huu huku ile mwaka 2018 ikitarajiwa kufanyika katika Pwani ya Dhahabu huko Australia.

No comments:

Post a Comment