Tuesday, April 1, 2014

BAYERN YAMNG'ANG'ANIA KROOS.

MWENYEKITI wa klabu ya Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge amesisitiza kuwa Toni Kroos hatajiunga na Manchester United msimu huu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 hajasaini mkataba mpya huku ule wa sasa ukitarajiwa kumalizika Juni mwaka 2015 na David Moyes alipigwa picha akiwa sambamba na wakala wa mchezaji huyo katika safari yake nchini Ujerumani aliyofanya Januari mwaka huu. Mapema mwezi uliopita Kroos alikataa kuondoa uwezekano wa kwenda United lakini Bayern sasa wameweka wazi kuwa kiungo huyo hataruhusiwa kuondoka mwishoni mwa msimu huu. Rummenigge alikaririwa akidai kuwa ana uhakika wa Kroos kuendelea kuvaa jezi ya Bayern kwa kipindi kirefu kijacho.

No comments:

Post a Comment