Tuesday, March 25, 2014

TAJIRI WA KIITALIANO AKATALIWA KUINUNUA LEEDS.

BODI ya Ligi nchini Uingereza imemuengua mfanyabiashara wa Italia Massimo Cellino kununua hisa kubwa katika klabu ya Leeds United. Cellino ambaye anamiliki kampuni ya michezo ya Eleonora, alikubali kununua hisa za asilimia 75 za timu hiyo kutoka Gulf Finance House Capital, Februari mwaka huu. Hata hivyo hatua yake hiyo ilitiliwa shaka wiki iliyopita wakati alipokutwa na hatia ya kushindwa kulipa ushuru wa boti yake ya kifahari. Tajiri huyo amesema ataka rufani kuhusiana na suala hilo ili aweze kuisaidia klabu hiyo ambayo ina matatizo ya kifedha hivi sasa.

No comments:

Post a Comment