Tuesday, April 29, 2014

BAYERN WATAIFUNGA MADRID - NEUER.

GOLIKIPA wa Bayern Munich, Manuel Neuer ana uhakika timu yake inaweza kutinga hatua ya fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuing’oa Real Madrid. Madrid waliibuka kidedea kwa kushinda bao 1-0 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Santiago Bernabeu wiki iliyopita na timu hizo zinatarajia kurudiana tena leo. Hata hivyo, Neuer anaamini kuwa uzoefu wa Bayern kutinga hatua hiyo utawasaidia kuifunga Madrid ambao wameshindwa kupenya kutoka katika hatua hiyo kwa misimu mitatu iliyopita. Neuer alitamba kuwa wana silaha zilizo katika hali nzuri na ana uhakika wataifunga Madrid.

No comments:

Post a Comment