Tuesday, April 29, 2014

TERRY, CECH FITI KUIVAA ATLETICO.

GOLIKIPA Petr Cech na beki John Terry wameanza mazoezi na timu yao leo kuelekea mchezo wa marudiano wa nusu fainali dhidi ya Atletico Madrid kesho. Ilisemekana Cech asingeweza kucheza tena msimu huu baada ya kuteua bega lake katika mchezo wa kwanza wakati Terry alitolewa nje kutokana na kuumia kifundo cha mguu katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya 0-0. Eden Hazard na Samuel Eto’o ambao walikuwa majeruhi wao pia walionekana kuwa fiti kwa kufanya mazoeziya leo. Viungo John Mikel Obi na Frank Lampard wote hawatakuwepo katika mchezo huo wa marudiano utakaofanyika katika Uwanja wa Stamford Bridge kutokana na kutumikia adhabu ya mechi moja.

No comments:

Post a Comment