Tuesday, April 29, 2014

KIPIGO CHAWAVURUGA MASHABIKI WA NEWCASTLE.

MENEJA wa klabu ya Newcastle United, Alan Pardew bado anaamini anaweza kubakia kwa muda mrefu kuifundisha timu hiyo pamoja na kupoteza mechi sita mfululizo na kusababisha mashabiki kuchukizwa. Mashabiki hao wa Newcastle wameonyesha hasira zao kufuatia kipigo cha mabao 3-0 walichopata kutoka kwa Arsenal jana usiku. Akihojiwa Pardew amesema anajua mashabiki hao wamehuzunishwa na kukasirishwa hivi sasa kwasababu hawajapa matokeo mazuri lakini ameomba uvumilivu kwani ana mipango ya muda mrefu na timu hiyo. Newcastle walianza vyema msimu mpaka kumalizika kwa mzunguko wa kwanza lakini walionekana kuporomoka toka kuanza kwa mwaka huu mpaka kufikia nafasi ya nane waliyopo hivi sasa.

No comments:

Post a Comment