Tuesday, April 29, 2014

WADHAMINI WA LA CLIPPERS WAJITOA KUTOKANA NA KAULI YA YA KIBAGUZI YA MMILIKI WAKE.

BAADHI ya wadhamini wa timu ya mpira wa kikapu ya Marekani, Los Angeles Clippers wamejitoa baada ya mmiliki wa timu hiyo kutuhumiwa kutoa kauli za kibaguzi. Chama cha Soka nchini humo-NBA inachunguza kauli hiyo ambayo inadaiwa kutolewa na Donald Sterling mwenye umri wa miaka 80. Wadhamini wanne ikiwemo kampuni ya Marcedes Benz ya Marekani wamesitisha udhamini wao wakati kampuni ya vinywaji ya Red Bull wakiwa mojawapo ya makampuni yaliyosimamisha matangazo yao. Wachezaji wa Clippers walifanya maandamano ya kimya kimya Jumapili kwa kuvaa fulana zao wakiwa wamezigeuza ndani-nje wakati wakipasha misuli yao moto kabla ya mechi dhidi ya Golden State Warriors.

No comments:

Post a Comment