Tuesday, April 29, 2014

REUS ACHOSHWA NA MASWALI YA MKATABA MPYA.

MSHAMBULIAJI wa Borussia Dortmund, Marco Reus amedai kuchoshwa na maswali kuhusu mustakabali wake na kukataa kuthibitisha kama amepewa ofa ya mkataba mpya. Kuna tetesi kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 amepewa ofa ya mkataba mpya ambao utaifanya thamani yake kupaa mpaka euro milioni 35 kwa timu nyingine itakayimhitaji. Hata hivyo, wakati akihojiwa kuhusiana na makubaliano hayo, Reus alikataa kusema chochote kuhusiana na suala hilo. Reus amesema hatasema chochote kuhusiana na mkataba wake lakini ana muda wa kuzungumzia kuhusu anavyojisikia vyema akiwa klabuni hapo.

No comments:

Post a Comment