Wednesday, May 21, 2014

FAINALI YA LIGI YA MABINGWA ULAYA MSIMU HUU INADHIHIRISHA UBORA WA LA LIGA - DI MARIA.

WINGA wa klabu ya Real Madrid, Angel Di Maria anaamini kuwa mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya Jumamosi dhidi ya Atletico Madrid unaelezea jinsi gani soka la Hispania lilivyokuwa na nguvu. Baadhi ya wachambuzi walidai kuwa fainali za michuano hiyo mwaka jana zilizohusisha timu za Ujerumani Bayern Munich na Borussia Dortmund zilikuwa dalili kuwa nchi hiyo ndiyo yenye nguvu kisoka. Hata hivyo, Di Maria anaamini ukweli kuwa La Liga ndio ligi bora umeonyeshwa msimu huu katika michuano ya Ulaya. Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina amesema fainali ya Ligi ya Mabingwa mwaka huu inaonyesha dhahiri kwa kiasi gani soka la Hispania lilivyokuwa. Di Maria amekiri itakuwa fainali nzuri na ngumu dhidi ya mahasimu wao hao wa jiji la Madrid lakini watajitahidi kufanya kila wanaloweza ili kuendeleza rekodi yao barani humo.

No comments:

Post a Comment