Friday, June 27, 2014

BOLT YUKO TAYARO KUSHIRIKI JUMUIYA YA MADOLA.

BINGWA mara sita wa michuano ya olimpiki, Usain Bolt amesema atakuwepo kwa ajili ya mashindano ya Jumuiya ya Madola inayotarajiwa kufanyika jijini Glascgow, Scotland baadae mwaka huu. Bolt mwenye umri wa miaka 27 raia wa Jamaica amesema anaweza asishiriki michuano ya mmoja mmoja lakini anaweza kukimbia katika mbio za kupokezana vijiti. Nyota huyo ambaye ameshinda medali za dhahabu katika mbio za mita 100, 200 na mita 400 kupokezana vijiti katika mashindano ya olimpiki mwaka 2008 na 2012, amekuwa akijiuguza majeraha ya mguu. Bolt aliandika katika mtandao wake kuwa yuko tayari kwa ajili ya uchaguzi kwa ajili ya michuano ya Jumuiya ya Madola na ameshapeleka nyaraka zote zinazohitajika. Hata hivyo mwanariadha huyo hatakuwa fiti vya kutosha kushiriki mashindano ya kufuzu michuano hiyo itakayofanyika mwishoni mwa wiki hii nchini Jamaica ingawa mwenye ana matumaini ya kuchaguliwa katika mbio za mita 400 kupokezana vijiti. Bolt hajawahi kushiriki michuano ya Jumuiya ya Madola baada ya kuikosa ile iliyofanyika jijini Melborne mwaka 2006 na ile iliyofanyika Delhi miaka minne iliyopita.

No comments:

Post a Comment