Tuesday, June 24, 2014

COSTA ACHOMOA KUIFUNDISHA CLERMONT.

KLABU ya Clermont Foot ya Ufaransa, imedai kuwa Helena Costa ameamua kutochukua mikoba ya kuifundisha timu hiyo msimu ujao. Costa mwenye umri wa miaka 36 raia wa Ureno amekuwa mwanamke wa kwanza kuteuliwa kufundusha timu ya wanaume barani Ulaya wakati alipoteuliwa kuchukua wadhifa huo Mei mwaka huu. Lakini rais wa klabu hiyo Claude Michy amesema mwanamama huyo ameamua kutoyatukuza majukumu yake na kuongeza kuwa uamuzi huo umekuwa wa ghafla na wa kushangaza. Sababu za Costa kukataa kibarua hicho bado hazijalikana. Kabla ya kukubali kibarua hicho cha kuinoa timu hiyo ya daraja la pili, Costa alikuwa kocha wa timu ya taifa ya wanawake ya Iran na pia likuwa akifanya kazi kama mng’amuzi wa vipaji wa klabu ya Celtic na kocha wa vijana wa Benfica ya Ureno.

No comments:

Post a Comment