Tuesday, June 24, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: ALVES AWAONYA WACHEZAJI WENZAKE KUTOBWETEKA.

BEKI mahiri wa timu ya taifa ya Brazil, Dani Alves amewaonya wachezaji wenzake kuwa baada ya kumaliza hatua ya makundi sasa michuano ya Kombe la Dunia ndio inaanza rasmi. Baada ya Brazil kuigaragaza Cameroon kwa kufunga mabao 4-1 jana na kumaliza kiongozi wa kundi A, beki huyo wa klabu ya Barcelona amesema hawatakiwi kufanya makosa kama waliyofanya katika mchezo huo ambapo yalipelekea Cameroon kusawazisha bao. Alves amesema sasa Kombe la Dunia linaanza baada ya kupita hatua ya makundi ambapo makosa yoyote yanaweza kufanyika yanaweza kuigharimu timu kuenguliwa katika michuano hiyo. Pamoja na hayo Alves amesema ushindi wlaiopata jana ulikuwa muhimu kwa kuwajenga wajiamini zaidi kwa ajili ya hatua ya inayoafuata ya mtoano. Brazil watakwaana na Chile katika hatua hiyo ya mtoano katika mchezo utakaochezwa Juni 28 mwaka huu huku washindi wa pili katika kundi lao Mexico wenyewe wkichuana na Uholanzi.

No comments:

Post a Comment