Tuesday, June 24, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: DEL BOSQUE AFIKIRIA KUACHIA NGAZI.

KOCHA wa timu ya taifa ya Hispania, Vicente del Bosque amesema anaweza kuamua mustakabali wake katika siku chache zijazo baada ya kumaliza ushiriki wao wa michuano ya Kombe la Dunia kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Australia. Mabingwa hao wa dunia wamemaliza katika nafasi ya tatu kwenye kundi B, baada ya kupata kipigo cha kushangaza kutoka kwa Uholanzi na Chile. Akiulizwa kuhusu mustakabali wake mara baada ya mchezo huo, Del Bosque amesema ataamua suala hilo katika siku chache zijazo au wiki ijayo kwani hana haraka na hilo. Hispania wameshinda Kombe la Dunia mwaka 2010 na michuano ya Ulaya mwaka 2012 wakiwa chini ya Del Bosque mwenye umri wa miaka 63. Kocha huyo amesema yeye pamoja na rais, katibu mkuu wa shirikisho la Soka la Hispania watazungumza kutafuta suluhisho zuri na watafanya kitu ambacho kitakuwa kizuri kwa maendeleo ya soka la nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment