Tuesday, June 24, 2014

OSCAR KUBAKIA CHELSEA MSIMU UJAO.

KIUNGO wa klabu ya Chelsea, Oscar amesema atabakia Stamford Bridge msimu ujao pamoja na kufanya mawasiliano na mabingwa wa Ufaransa Paris Saint-Germain-PSG. Kwa muda mrefu PSG imekuwa ikimhusudu nyota huyo wa kimataifa wa Brazil, huku meneja wake Laurent Blanc akisema wazi wazi na kumekuwa na tetesi kuwa kiungo huyo anaweza kumfuata David Luiz huko. Nafasi ya Oscar, Chelsea imekuwa mashakani kufuatia kuwasili kwa Cesc Fabregas wakati kumekuwa na mashaka pia ya kuporomoka kw akiwango cha kiungo huyo msimu uliopita. Lakini wakati Oscar akikiri kuwasilina na PSG, amesema hakuna maafikiano yoyote yaliyofikiwa hivyo ataendelea kuwepo Stamford Bridge msimu ujao.

No comments:

Post a Comment