Tuesday, June 24, 2014

YAYA TOURE AWASHAMBULIA VIONGOZI WA CITY KWA KUMKATALIA KWENDA KUMUONA NDUGUYE HOSPITALI.

KIUNGO mahiri wa kimataifa wa Ivory Coast Yaya Toure amebainisha kusikitishwa na klabu ya Manchester City kumkatalia kumpa kibali ili kwenda kumuona mdogo wake alipokuwa amelazwa wakati alipokwenda Abu Dhabi. Ibrahim Toure ambaye alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya saratani alifariki akiwa na umri wa miaka 28 wiki iliyopita wakati kama zake Yaya na Kolo wakiwa katika majukumu ya kimataifa na Ivory Coast katika michuano ya Kombe la Dunia. Kiungo huyo wa zamani wa Barcelona, hata hivyo amesema City hawakumpa ruhusa ya kwenda kumtembelea ndugu yake huyo hospitali muda mfupi baada ya kufanikiwa kunyakuwa taji la Ligi Kuu. Badala yake kikosi cha City kilisafiri kwenda Abu Dhabi kucheza na klabu ya Al-Ain ikiwa ni sehemu ya sherehe za ubingwa wao. Yaya amesema alikuwa akisikia vibaya kwenda kusheherekea taji la ligi wakati kaka yake afya ikizidi kudhoofika hata hivyo maofisa wa City walikuwa akijua hilo lakini hawakumpa ruhusa aliyohitaji.

No comments:

Post a Comment