Tuesday, June 24, 2014

UNITED YAMTENGEA HERRERA PAUNDI MILIONI 30.

KLABU ya Manchester United inajipanga kutenga kitita cha paundi milioni 30 kwa ajili ya kumsajili Ander Herrera kutoka klabu ya Athletic Bilbao. United walishindwa kumsajili kiungo huyo wa kimataifa wa Hispania mwenye umri wa miaka 24 katika muda wa mwisho wa usajili kiangazi mwaka jana. Lakini meneja mpya Loius van Gaal amemua kujaribu tena kumsajili kiungo huyo katika dili ambalo pengine likakamilika Jumanne ijayo. Herrera ambaye alikuwa katika kikosi cha Hispania kilichoshiriki michuano ya olimpiki iliyofanyika London mwaka 2012 anatarajiwa kuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Van Gaal toka Mholanzi huyo alipochukua nafasi ya David Moyes Juni mwaka huu. Toka aliposajiliwa Marouane Fellaine kutoka Everton kiangazi mwaka jana, United walikuwa hawajasajili mchezaji anayecheza nafasi ya kiungo wakati kwa miaka sita.

No comments:

Post a Comment