Tuesday, June 24, 2014

RATIBA YA BUNDESLIGA YATOKA.

BAADA ya kutoka ratiba ya Ligi Kuu nchini Uingereza, sasa imekuwa zamu ya Ujerumani kwa kutoa ratiba yao Bundesliga kwa ajili ya msimu ujao wa 2014-2015. Mabingwa wa Bundesliga kwa misimu miwili mfululizo, Bayern Munich wanatarajiwa kuanza kutetea taji lao nyumbani huko Allianz Arena kwa kuchuana na Wolfsburg Agosti 22 mwaka huu. Mahasimu wao Borussia Dortmund wao watafungua dimba na Bayer Leverkusen wakati Schalke wao watasafiri kuifuata Hannover wakati timu zilizopanda daraja msimu huu Koln na Paderborn zenyewe zitapambana na Humburg na Mainz. Mechi ya kwanza itakayozikutanisha mahasimu wa jiji Dortmund na Schalke itachezwa mwishoni mwa wikiendi ya mwisho ya mwezi Agosti wakati Bayern wao wataikaribisha Dortmund mwishoni mwa mwezi Octoba huku ile ya marudiano ikitarajiwa kuchezwa kati ya Mei 4 au 5 mwakani. Msimu utakamalizika kwa mabingwa watetezi Bayern kumaliza na Mainz huku mahasimu wao Dortmund wao wakimaliza na Werder Bremen.


No comments:

Post a Comment