Thursday, June 26, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: MESSI ANATOKEA SAYARI YA JUPITER - KESHI.

KOCHA wa timu ya taifa ya Nigeria, Steven Keshi amesema Lionel Messi ametokea sayari ya Jupiter baada ya Muargentina huyo kufunga mabao mawili katika ushindi wa mabao 3-1 waliopata dhidi ya wawakilishi hao wa bara la Afrika. Messi mwenye umri wa miaka 27 alifunga mabao hayo ambayo yameifanya Argentina kumaliza kinara katika kundi F. Keshi amesema ni mmoja mchezaji wa kipekee, amejaaliwa kipaji na hakuna mtu anayeweza kuchukua hilo kutoka kwake. Pamoja na kufungwa Nigeria walifanikiwa kufuzu hatua inayofuata baada ya Iran kushindwa kutamba mbele ya Bosnia-Herzegovina na sasa mabingwa hao wa Afrika watachuana na vinara wa kundi E ambao ni Ufaransa katika hatua hiyo. Argentina wao wameangukia kwa Swizterland aliyemaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi E baada ya kuitandika Honduras kwa mabao 3-0.

No comments:

Post a Comment