Tuesday, June 24, 2014

SINA UHAKIKA NA KUMSTAKABALI WANGU MADRID - DI MARIA.

WINGA Angel Di Maria amekiri kuwa hana uhakika na mstakabali wake katika klabu ya Real Madrid, kufuatia timu za Ligi Kuu kuonyesha nia ya kumsajili. Winga huyo mwenye umri wa miaka 26 aekuwa akihusishwa na tetesi za kuhama baada ya kuwa na msimu mzuri Madrid ambapo amefunga mabao 11 na kusaidia mengine 26 hivyo kuingoza timu hiyo kunyakuwa taji la La Liga na Ligi ya Mabingwa Ulaya. Arsenal na Manchester United zimeonekana kufuatilia kwa karibu kiwango cha winga huyo katika michuano ya Kombe la Dunia akiwa na timu yake ya taifa ya Argentina ambapo amecheza katika mechi zote mbili dhidi ya Bosnia na Iran. Hata hivyo, Di Maria amesema kwasasa amehamishia mawazo yake kwa nchi yake kwenye michuano hiyo lakini akakiri kuwa hana uhakika na mustakabali wake Madrid. Akihojiwa Di Maria amesema hajui kitakachotokea kwasasa na hana uhakika wa maisha yake ya soka huko mbele kwasababu nguvu na mawazo yake ameyaweka katika timu yake ya taifa ila baada ya michuano hiyo ndio atajua kitakachotokea.

No comments:

Post a Comment