Sunday, June 22, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: DANI ALVES AMPONDA SHEARER.

BEKI mahiri wa kimataifa wa Brazil, Dani Alves amemshambulia Alan Shearer kwa kudai kauli ya mchambuzi huyo wa soka wa BBC kuhusu mshambuliaji Fred ni ya kipuuzi. Mshambuliaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Uingereza aliiambia luninga ya ESPN wiki iliyopita kuwa chaguo la kwanza la mshambuliaji wa kati wa Brazil hana kasi na hawezi kupiga mashuti hivyo anatakiwa kuondolewa katika kikosi cha kwanza cha nchi hiyo. Pamoja na kuwa na rekodi nzuri ya kufunga kwa Brazil mwaka uliopita, Fred ambaye anacheza katika timu ya Fluminense amekuwa kimya sana katika michuano hii kwa kushindwa kufumania nyavu katika mechi mbili walizocheza. Shearer amesema hajui kwanini Brazil bado wanaendelea kumpanga katika kikosi cha kwanza kwnai hana msaada wowote katika safu ya ushambuliaji. Lakini Alves alimshambulia vikali Shearer kwa kauli hiyo nakudai kuwa ni ya kipuuzi kwa mtu ambaye amecheza soka na anayejua ugumu wa suala ufungaji kwa mchezaji. Brazil kwasasa wanaongoza katika kundi A kuelekea mchezo wao mwisho dhidi ya Cameroon huku timu itakayoongoza kundi ikitarajiwa kupambana na aidha Chile au Uholanzi katika hatua ya timu 16 bora.

No comments:

Post a Comment