Thursday, June 26, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: JAPAN YAANZA MCHAKATO WA KOCHA MPYA BAADA YA ZACCHERONI KUACHIA NGAZI.

CHAMA cha Soka nchini Japan, kimeanza mchakato wa kutafuta kocha mpya baada ya Alberto Zaccheroni kuamua kuachia ngazi kutokana na kushinda kuipa ushindi nchi hiyo katika michezo ya hatua ya makundi. Vyombo vya habari nchini Japan vimeripoti kuwa kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Mexico Javier Aguirre ndiye anayepewa nafasi ya kuchukua mikoba hiyo. Taarifa hizo ziliendelea kudai kudai kuwa tayari JFA wameshaanza mazungumzo na kocha huyo mkongwe ambaye aliliongoza taifa lake kufika hatua ya timu 16 bora mara mbili katika michuano ya mwaka 2002 na 2010. Japan walikwenda katika michuano hiyo inayoendelea nchini Brazil wakia na matumani baada ya kufuzu kirahisi katika hatua ya makundi huku wakitabiriwa kufika hatua ya robo fainali lakini hayakwenda kama walivyotaraji kwani walijikuta wakiondolewa katika hatua ya mwanzo. Kipigo kutoka kwa Ivory Coast na Cololmbia pamoja na sare dhidi ya Ugiriki yalitosha kuifanya timu hiyo kuburuza mkia katika kundi C.

No comments:

Post a Comment