Thursday, June 26, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: UBELGIJI KUWAKOSA KOMPANY NA VERMAELEN KATIKA MCHEZO WA LEO.

KOCHA wa timu ya taifa ya Ubelgiji, Marc Wilmots amedai kuwa watacheza mchezo wao wa mwisho wa mwisho wa kundi H dhidi ya Korea Kusini baadae leo bila ya kuwa na nahodha wake Vincent Kompany na Thomas Vermaelen. Wilmots aliwaambia waandishi wa habari kuwa kila kitu kilikuwa kinakwenda sawa lakini wana wachezaji wenye majeruhi madogo mdogo hivyo watawapumzisha katika mchezo dhidi ya Korea Kusini. Vermaelen alitegemea kuukosa mchezo huo baada ya kutolewa nje mapema katika mchezo wa Jumapili iliyopita walioshinda bao 1-0 dhidi ya Urusi wakati Kompany yeye alijitonesha maumivu ya msuli wakati akiwa katika mazoezi. Ubelgiji tayari wamefuzu hatua ya timu 16 bora lakini watahitaji kupata alama ili kujihakikishia nafasi ya kumaliza vinara katika kundi lao la G.

No comments:

Post a Comment