Thursday, June 26, 2014

MAN UNITED BADO WAWEKA MATUMAINI KWA HERRERA PAMOJA NA KUKATALIWA OFA YAO YA KWANZA.

KLABU ya Manchester United bado ina matumaini ya kumsajili kiungo wa Athletic Bilbao Ander Herrera pamoja na ofa yao ya oaundi milioni 29 kukataliwa na timu hiyo. Inadaiwa kuwa United imefikia bei iliyowekwa katika mkataba wa Herrera lakini Bilbao bado wanaonekana kuhitaji fedha zaidi kwa ajili ya kumuuza mcezaji huyo. Mara ya kwanza United walishindwa kumnunua kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 katika kipindi cha usajili majira ya kiangazi mwaka jana lakini meneja mpya Louis van Gaal ameonekana kufufua upya suala hilo. Lakini pamoja na hayo United bado wana matumaini ya kumsajili kiungo huyo kabla ya kuanza kwa ziara ya zao za maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu zinazotarajiwa kuanza Julai 18 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment