Thursday, June 26, 2014

MAN CITY YANASA KIUNGO KUTOKA PORTO.

KLABU ya Manchester City imekamilisha usajili wa kiungo wa kimataifa wa Brazil Fernando kutoka klabu ya FC Porto ya Ureno. Porto ilitangaza taarifa hizo katika soko la hisa la Lisbon jana baada ya kukubali kuchukua kitita cha paundi milioni 12 kutoka City. City wamethibitisha uhamisho huo leo ingawa hawakueleza wamempa nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 mkataba wa miaka mingapi. Akihojiwa Fernando amesema amefurahishwa na usajili na atajitolea kwa nguvu zake zote kuisaidia klabu hiyo ya Manchester. Fernando amejiunga na Porto mwaka 2007 ambapo ameshinda mataji manne la Ligi pamoja na moja la Europa League mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment