Thursday, June 26, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: MUNTARI, BOATENG WATIMULIWA KWA UTOVU WA NIDHAMU.

WACHEZAJI Sulley Muntari na Kevin-Prince Boateng wametimuliwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Ghana kufuatia tuhuma za utovu wa nidhamu. Katika taarifa iliyotumwa katika mtandao wa Chama cha Soka cha nchi hiyo-GFA, zimeeleza kuwa Boateng alitimuliwa kwa kutumia lugha ya kudhalilisha kwa kocha Kwesi Appiah wakati Muntari yeye alitishia kumpiga mjumbe wa kamati ya utendaji ya GFA. Taarifa hizo zimetoka muda mchache kabla ya mchezo wao dhidi ya Ureno ambao unaendelea hivi muda huu. Black Stars bado wana nafasi ya kufuzu hatua inayofuata kama wakifanikiwa kuifunga Ureno huku wakiomba Ujerumani iifunge Marekani katika mchezo mwingine ambao nayo unachezwa hivi sasa.

No comments:

Post a Comment