Thursday, June 26, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: SUAREZ AFUNGIWA MIEZI MINNE KUJISHUGHULISHA NA SOKA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Uruguay, Luis Suarez amefungiwa kujishughulisha na masuala yoyote yanayohusiana na soka kwa miezi minne kwa kumng’ata beki wa timu ya taifa ya Italia Giorgio Chiellini. Nyota huyo wa Liverpool mwenye umri wa miaka 27 pia amefungiwa kucheza mechi za kimataifa tisa, hivyo kumfanya kuikosa michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu. Hatua hiyo pia itamfanya kukosa mechi tisa za Ligi Kuu ya Uingereza msimu ujao. Tukio la kumng’ata Chiellini lililotokea Jumanne iliyopita katika mchezo wa kundi D ambao Uruguay ilishinda na kuvuka katika hatua ya timu 16 bora. Uruguay imepewa siku tatu za kukata rufani dhidi ya adhabu hiyo. Adhabu ni kubwa zaidi katika historia ya michuano ya Kombe la Dunia, ambapo imeizidi ile ya kufungiwa mechi nane aliyowahi kupewa Mauro Tassotti wa Italia kwa kumpiga kiwiko mchezaji wa Hispania Luis Enrique mwaka 1994.


No comments:

Post a Comment