Friday, June 27, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014; TIMU ZILIZOTINGA HATUA YA 16 BORA.

TIMU za Afrika zilizofuzu 16 Bora ya Kombe la Dunia nchini Brazil zitakutana na mabingwa wa zamani wa michuano hiyo katika hatua hiyo. Nigeria itamenyana na Ufaransa wakati Algeria itamenyana na Ujerumani ambapo kama wakifanikiwa kushinda watakuwa wameungana na Cameroon, Senegal na Ghana katika orodha ya timu za Afrika zilizowahi kufika robo fainali ya Kombe la Dunia. Mechi nyingine za Robo Fainali ni kati ya Brazil na Chile, Colombia na Uruguay, Uholanzi na Mexico, Argentina na Uswisi na Ubelgiji na Marekani. Michezo hiyo ya mtoano inatarajiwa kuanza kutimua vumbi kesho ambapo wenyeji Brazil watakuwa wakipepetana na Chile mchezo ambao utachezwa saa moja usiku ukifuatiwa na mchezo kati ya Colombia na Uruguay utakaochezwa saa tano za usiku.

No comments:

Post a Comment