Monday, June 30, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: KLM YAOMBA RADHI MASHABIKI WA MEXICO KWA KUTUMA UJUMBE WA UTANI KWENYE AKAUNTI YAKE RASMI YA TWITTER.

SHIRIKA la Ndege la Uholanzi, KLM limeomba radhi kwa kutuma ujumbe kwenye ukurasa wake rasmi wa mtandao wa kijamii wa twitter kuwatania Mexico kutokana kipigo walichopata kutoka kwa Uholanzi kwenye michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Brazil. Ndani ya muda wa dakika chache kutoka Uholanzi ipate ushindi wa mabao 2-1 katika dakika za majeruhi, kulitumwa picha yenye bando la kuondoka huku kukiwa na kichwa cha habari kilichosomeka kwa lugha ya kireno Adios Amigos wakimaanisha Kwaherini Marafiki. Pembeni ya bango hilo la kuondokea kukawekwa picha wa mtu akiwa na mstachi pamoja na kofia kubwa aina ya sombrero ikieleza uhahilisia wa watu wa Mexico lakini muda mfupi baadae walifunta ujumbe huo. Mwigizaji maarufu wa Mexico Gael Garcia Bernal naye aliandika katika ukurasa wake wa twitter akiwahabalisha mashabiki zaidi ya milioni mbili wanaomfuata kuwa hatasafiri tena kwa ndege za shirika hilo na mamia ya watu kuonekana kulalamikia tukio hilo. Msemaji wa KLM Lisette Ebeling Koning baadae aliwaambia waandishi wa habari kuwa ujumbe ule ulikuwa ni wa utani lakini watu wengi wameochukulia tofauti. Koning aliendelea kudai haikuwa nia ya shirika hilo kuwaudhi watu wa Mexico ambao wanawahudumia kwa ndege ya kila siku ya shirika hilo kati ya Mexico City na Amsterdam na kuwaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.

No comments:

Post a Comment