Monday, June 30, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: KOCHA WA ALGERIA AKWEPA KUULIZWA MASWALI YA MFUNGO WA RAMADHANI KWA WACHEZAJI WAKE.

KOCHA wa timu ya taifa ya Algeria, Vahid Halilhodzic kubainisha ni wachezaji gani waislamu katika kikosi chake ambao watafunga mwezi mtukufu wa Ramadhani katika mchezo wa mtoano dhidi ya Ujerumani utakaochezwa baadae leo usiku. Siku thelathini za mfungo wa Ramadhani zimeanza jana na kocha huyo mwenye umri wa miaka 30 alionekana kukwepa maswali kuhisiana na suala hilo wakati wa mkutano wake na waandhisi wa habari. Kocha huyo raia wa Bosnia amesema suala hilo ni la binafsi zaidi na wakati ukiluliza swali hilo unakuwa unakosa heshima na maadili. Halilhodzic aliendelea kudai kuwa hawezi kuingilia imani ya mchezaji yeyote kwani wanaweza kufanya watakavyoataka. Kufunga Ramadhani kwa waislamu ni moja kati ya nguzo muhimu za dini hiyo, ingawa kuna baadhi ya watu kama wagonjwa, wajawazito, wasiojiweza na wazee ambao wanaruhisiwa kutokufunga. Nahodha wa Algeria Madjid Bougherra ameeleza kuwa atafunga mwezi huu mtukufu lakini kiungo wa Ujerumani Mesut Ozil na beki wa Ufaransa Bacary Sagna wote wamedai kuwa hawatafunga.

No comments:

Post a Comment