Monday, June 30, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: MOURINHO AUNGA MKONO ADHABU YA WALIYOTOA FIFA DHIDI YA SUAREZ.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amedai kutokubaliana na adhabu ya kumfungia Luis Suarez kwenda uwanjani kufuatia nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay kumng’ata beki wa Italia Giorgio Chiellini. Mourinho amekubaliana na adhabu ya kutocheza kwa muda aliyopewa mshambuliaji huyo wa Liverpool lakini haoni tatizo kwa Suarez kuhudhuria uwanjani kutizama mechi. Akizungumza na mtandao wa Yahoo, Mourinho ambaye pia kuzinoa timu za Reala Madrid na Inter Milan amesema Suarez alistahili adhabu aliyopewa kutokana na kurudia tukio hilo mara kwa mara ila kitu ambacho hakikumfurahisha na kumfungia kwenda uwanjani kuangalia timu yake ikicheza.

No comments:

Post a Comment