Monday, June 30, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: RAIS WA URUGUAY AWATUSI FIFA.

RAIS wa Uruguay Joe Mujica amewatolea maneno ya kuwatusi viongozi wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kutokana na kumfungia Luis Suarez kujishughulisha na shughuli zozote za kimichezo kwa miezi minne. Rais huyo mwenye umri wa miaka 79 aliielezea adhabu hiyo ambayo pia inahusisha kumfungia nyota huyo mechi tisa za kimataifa kuwa ya mabavu. Suarez alipewa adhabu hiyo ambayo ni kali zaidi katika historia ya Kombe la Dunia kwa kosa la kumng’ata beki wa Italia Giorgio Chiellini. Mujica anajulikana kwa tabia yake ya kuzungumza kile anachojikia mahali popote bila ya uoga. Rais huyo alitoa kauli hiyo katika luninga wakati wa mapokezi ya timu ya taifa ya nchi hiyo kufuatia kuondolewa katika hatua ya timu 16 bora na Colombia ambapo mara baada ya kutoa lugha hiyo ya matusi alishika mdomo lakini aliwaruhusu waandishi wa habari kuitoa kauli hiyo kama ilivyo.


No comments:

Post a Comment