Tuesday, July 1, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: FIFA YAMSIMAMISHA OFISA HABARI WA BRAZIL.

OFISA habari wa Shirikisho la Soka la Brazil, Rodrigo Paiva amesimamishwa na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kufuatia tukio la kumpiga mchezaji wa Chile Mauricio Pinilla wakati wa mchezo baina ya timu hizo uliochezwa Jumamosi iliyopita. Paiva anatarajiwa kuukosa mchezo wa Ijumaa wa robo fainali utakaikutanisha Brazil na Colombia kutokana na FIFA kuendelea na uchunguzi wa tuhuma za kumpiga Pinilla katika muda wa mapumziko. Paiva amejitetea kuwa alikuwa akijilinda kwa kumsukuma mchezaji huyo wakati alipomkaribia, wakati wakienda katika vyumba vya mapumziko. Katika mchezo huo Brazil ilifanikiwa kuifunga Chile kwa changamoto ya mikwaju ya penati baada ya timu hizo kutoka sare ya kufungana bao 1-1 katika muda wa kawaida na wa nyongeza.

No comments:

Post a Comment