Tuesday, July 1, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: KESHI AAMUA KUACHIA NGAZI BAADA YA KIPIGO CHA UFARANSA.

KOCHA wa timu ya taifa ya Nigeria, Stephen Keshi amejiuzulu wadhfa wake huo mara baada ya imu hiyo kuondolewa katika michuano ya Kombe la Dunia kwa kufungwa mabao 2-0 na Ufaransa. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 52 alichukua mikoba ya kuinoa Super Eagles mwaka wa 2011 na akaiongoza timu hiyo kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka jana. Nahodha wa timu hiyo Joseph Yobo aliyejifunga bao la pili kwenye mchezo huo naye pia ametangaza kustaafu. Chini ya uongozi wake Super Eagles imefuzu kwa mara ya kwanza hatua ya mtoano katika michuano hiyo toka walipofanya hivyo mwaka 1998, licha ya migomo ya mara kwa mara ya wachezaji wake wakidai malimbikizo ya posho zao. Kujiuzulu kwa Keshi kunafanya idadi ya makocha waliojiuzulu kufuatia matokeo duni ya timu zao katika michuano ya Kombe la Dunia kufikia sita. Makocha wengine waliondoka ni pamoja na Luis Suarez wa Honduras, Carlos Queiroz wa Iran, Alberto Zaccheroni wa Japan , Cesare Prandelli wa Italia na Sabri Lamouchi wa Ivory Coast.

No comments:

Post a Comment