Friday, June 27, 2014

WADHAMINI WAANZA KUMKIMBIA SUAREZ KWA UPUUZI WAKE.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Uruguay Luis Suarez amempoteza mmoja wa wadhamni wake baada ya kufungiwa na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kwa kumng’ata beki Giorgio Chiellini wa Italia. Kampuni ya kamari katika mtandao ya 888poker wamesema wameamua kusitisha mahusiano yao na mchezaji huyo kutokana na tukio lake hilo. Suarez mwenye umri wa miaka 27 ambaye pia ancheza katika klabu ya Liverpool amefungiwa miezi minne kujishughulisha na masuala ya soka kutokana na tukio hilo. Adhabu hiyo itamfanya Suarez kutocheza soka kwa nchi yake au klabu mpaka mwishoni mwa Octoba mwaka huu. Uruguay inatarajiwa kucheza na Colombia katika hatua ya timu 16 bora kesho baada ya kufuzu kutoka katika kundi B nyuma ya Costa Rica. Mbali na adhabu hiyo, FIFA pia imefungia mchezaji huyo mechi tisa za kimataifa huku akitozwa faini ya euro 82,000.

No comments:

Post a Comment