Sunday, July 27, 2014

BAYERN WAMUHAKIKISHIA KIBARUA GUARDIOLA.

OFISA mkuu wa klabu ya Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge amewahakikishia mashabiki kuwa Pep Guardiola hatatimuliwa na klabu hiyo. Januari mwaka 2007 Bayern walimtimua kocha wao Felix Magath wakati Louis van Gaal naye alitimuliwa April mwaka 2011 kutoka na kusuasua kwa timu hiyo vipindi hivyo. Lakini Rummenigge amewahakikishia mashabiki kuwa jambo kama halitaweza kutokea safari na Guardiola anatakiwa kuwa na uhakika wa kibarua chake. Rummenigge aliongeza kuwa Guardiola bado ataendelea kuwa kocha wa Bayern mpaka Juni 30 mwaka 2016 kama mkataba unavyoeleza.

No comments:

Post a Comment