Sunday, July 27, 2014

FALCAO KUSHIRIKI MICHUANO YA KOMBE LA EMIRATES WIKI IJAYO.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Colombia na klabu ya Monaco, Radamel Falcao anatarajiwa kurejea uwanjani mwishoni mwa wiki ijayo katika michuano ya Kombe la Emirates inayoandaliwa na klabu ya Arsenal. Falcao mwenye umri wa miaka 28 alipata majeruhi ya goti katika mchezo wa Kombe la Ligi nchini Ufaransa, Januari 26 hivyo kulazimika kuikosa michuano ya Kombe la dunia iliyofanyika nchini Brazil. Meneja wa klabu ya Monaco Leonardo Jardim amesema nyota huyo kwasasa yuko katika hatua za mwisho ili aweze kupona kabisa hivyo anadhani atakuwepo katika michuano hiyo itakayofanyika jijini London. Pamoja na tetesi za nyota huyo kwenda klabu ya Real Madrid, Jardim amesema kwasasa anajua Falcao bado ni mchezaji wa Monaco na amemuweka katika mipango yake. Monaco, Valencia na Arsenal watachuana katika michuano ya Kombe la Emirates itakayofanyika jijini London Agosti 2 na 3.

No comments:

Post a Comment