Sunday, July 27, 2014

SERENGETI BOYS KWENDA AFRIKA KUSINI KESHO.

KIKOSI cha wachezaji 19 cha timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17, Serengeti Boys kinatarajiwa kuondoka kesho kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya mechi dhidi ya Afrika Kusini. Mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya pili itachezwa Jumamosi, Agosti 2 mwaka huu kwenye Uwanja wa Dobsonville uliopo Soweto, Johannesburg kuanzia saa 9 kamili mchana kwa saa za Afrika Kusini. Katika mchezo wa kwanza uliofanyika kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam timu hizo zilitoka suluhu. Mshindi katika mchezo huo atacheza raundi ya mwisho ya michuano hiyo ya Afrika na mshindi wa mechi kati ya Misri na Congo Brazzaville. Fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 zitafanyika mwakani nchini Niger.


No comments:

Post a Comment