Wednesday, July 30, 2014

EL HILAL YAMTIMUA KOCHA BAADA YA KIPIGO.

KLABU ya El Hilal ya Sudan imetangaza kumtimua kocha wake Mbrazil Paulo Campos kufuatia tabia mbovu wakati wa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika mzunguko wa nne hatua ya makundi waliofungwa na AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo uliochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita. Katika mchezo huo wa ugenini waliocheza jijini Kinsasha, Al Hilal ilikuwa imepata sare ya bao 1-1 dhidi ya Vita lakini penati ilitolewa dakika za mwisho kwa wenyeji na kusababisha Campos kushindwa kuzuia jazba na kumvamia mwamuzi. Campos alikimbia kuingia uwanjani na kufuatiwa na wachezaji kumlalamikia mwamuzi kwa penati hiyo, tabia ambayo uongozi wa Hilal baadae waliikemea vikali katika taarifa yao. Baada kufanya kikao cha dharura bodi ya klabu hiyo iliamua kusitisha mkataba wa kocha huyo kwasababu ya tabia mbovu na kuonyesha mfano mbaya kwa wachezaji anaowaongoza. Katika mchezo huo Hilal ilitandikwa mabao 2-1 na sasa wanashika nafasi ya tatu katika kundi A linaloongozwa na TP Mazembe wakifuatiwa na AS Vita wote wakiwa wamefungana alama huku Zamalek wakiburuza mkia.

No comments:

Post a Comment