Wednesday, July 30, 2014

ZAMALEK YAMTIMUA MIDO.

KLABU kongwe ya Misri, Zamalek imemtimua kocha wake Ahmed Hossam maarufu kama Mido na wanatarajiwa kutangaza kocha mpya katika kipindi kifupi kijacho. Mido alichukua mikoba ya kuinoa timu hiyo Januari mwaka huu akichukua nafasi ya Helmy Tolan aliyetimuliwa kutokana na matokeo mabovu. Mido aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter kuwa mjumbe wa bodi wa klabu hiyo Ahmed Soliman alimpigia simu na kumpatia taarifa hizo za kusitisha mkataba wake. Bodi ya klabu hiyo ilikutana jana na kufikia maamuzi ya kumtimua kocha na kuajiri mwingine atakayeingoza timu hiyo kwa ajili ya mechi zao zote za Ligi ya Mabingwa Afrika zilizobakia pamoja na msimu mpya wa Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment