Wednesday, July 30, 2014

TOURE ATHIBITISHA KUBAKIA MAN CITY.

KIUNGO wa klabu ya Manchester City, Yaya Toure amesema anataka kubakia klabuni hapo kwa kipindi kirefu kijacho. Kumekuwa na taarifa katika kipindi hiki cha kiangazi kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 31 alikuwa hana furaha Etihad huku wakala wake Dimitry Seluk akidai Toure anafikiri haheshimiwi na mabosi wa mabingwa hao wa Ligi Kuu. Lakini Toure ameuambia mtandao wa klabu hiyo kuwa hakuwa na nia ya kuondoka kwani amemua kubakia hapo kwa kipindi kirefu kadri atakavyoweza. Seluk alilalama kuwa siku ya kuzaliwa ya mteja wake ilidharauliwa na mabosi wake wakati kikosi cha timu hiyo kilipokwenda Abu Dhabi kwa ajili ya kushangilia taji lao la ligi Mei mwaka huu. Baadae Seluk aliiambia BBC kuwa mteja anataka kuhakikishiwa kibarua chake pamoja na kuudhiwa na jinsi alivyofanyiwa.

No comments:

Post a Comment