Wednesday, July 30, 2014

MICHUANO YA YA KOMBE LA COSAFA YAFUTWA.

BARAZA la Michezo kwa nchi za Kusini mwaka Afrika-COSAFA limetangaza kuwa michuano ya Kombe la Cosafa ambayo ilikuwa ifanyike nchini Botswana kuanzia Septemba 13 hadi 28 mwaka huu imefutwa. Rais wa Cosafa Seketu Patel amesema kwasasa wako katika mchakato wa kutafuta mwenyeji mwingine kwa ajili ya kuandaa michuano hiyo. Patel amesema wamelazimika kufuta michuano hiyo kutokana na matatizo ya kifedha na miundo mingine ya kuwezesha michuano hiyo kuchezwa. Rais huyo amesema kwasasa wanasubiria maombi yao waliyotuma na kuahidiwa kupewa mwishoni mwa wiki hii kabla ya kutoa taarifa rasmi kwa vyombo vya habari.

No comments:

Post a Comment