Wednesday, July 30, 2014

KEITA AENDELEZA BIFU LAKE NA PEPE.

BIFU la wachezaji Seudou Keita na Pepe limeibuka upya baada ya Keita anayecheza AS Roma kushindwa kushikana na mikono na Pepe kabla ya kuanza kwa mchezo wa kirafiki dhidi ya Real Madrid jijini Dallas. Keita alimpotezea Pepe kwa kumnyima mkono wake na badaae kutupa chupa iliyoonekana kumgonga beki huyo wa kimataifa begani. Wawili hao wamekuwa na bifu toka Keita akiwa anaitumikia Barcelona ambapo mshambuliaji huyo wakimataifa wa Mali alimtuhumu Pepe kwa kunfanyia vitendo vya ubaguzi wa rangi katika mchezo wa Super Cup nchini Hispania mwaka 2011. Pepe ambaye amehusika katika matukio kadhaa yenye utata, alionekana kutulia jana na hata kucheka wakati chupa hiyo ilipompiga begani. Katika mchezo huo Roma iliitandika Madrid bao 1-0.


No comments:

Post a Comment