Thursday, July 31, 2014

GASGOW 2014: SIKU YA NANE MICHUANO YA MADOLA TANZANIA BADO BILABILA.

WAKATI michuano ya Jumuiya ya Madola inayoendelea jijini Glasgow, Scotland ikiingia siku yake ya nane leo, Tanzania imeendelea kuboronga kwa kushindwa kuambulia walau medali moja. Baada ya kuchemka katika michezo ya ngumi, meza, judo na kuogelea sasa itakuwa zamu ya wanariadha ambapo Dotto Ikangaa na Brazili John watakuwa na kibarua kigumu cha kuhakikisha wanafuzu katika fainali yam bio za mita 1,500. Mpaka sasa Uingereza ndio wanaoongoza katika orodha ya medali kwa kujizolea 105, dhahabu 38, fedha 35 na shaba 32 wakifuatiwa na Australia waliojizolea medali 106, dhahabu 35, fedha 32 na shaba 39 huku Canada wao wakishika nafasi ya tatu kwa kuzoa medali 51 dhahabu 22 fedha saba na shaba 22. Kwa upande wa Afrika, Afrika Kusini ndio wanaoondoza kwa kuchukua medali nyingi ambapo mpaka wameshachukua medali 31, dhahabu tisa fedha 10 na shaba 12 wakifuatiwa na Nigeria waliozoa medali 19, dhahabu sita, fedha tano na shaba nane. Kenya ndio walioitoa kimasomaso Afrika Mashariki kwa kuzoa medali 12 mpaka sasa ambapo tano kati ya hizo ni dhahabu, tano zingine za fedha na mbili shaba huku Uganda wakifuatia kwa kuambulia medali moja ya shaba.

No comments:

Post a Comment