Monday, July 28, 2014

ETO'O APEWA OFA YA KUJIUNGA NA WEST HAM.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Chelsea, Samuel Eto’o amepewa ofa ya kujiunga na klabu ya West Ham United lakini nyota huyo mwenye umri wa miaka 33 anahitaji kulipwa kitita cha paundi 100,000 kwa wiki. Meneja wa West Ham Sam Allardyce ambaye anataka mshambuliaji mbadala baada ya Andy Carroll kuumia pia ameonyesha nia ya kumtaka Joel Campbell ambaye anawindwa na AC Milan. Kwasasa Wst Ham imeanza mazungumzo na Hugo Almeida mwenye umri wa miaka 30 ambaye ni mchezaji huru lakini naye anataka mshahara wa paundi milioni 2.5 kwa mwaka. Kwa upande mwingine West Ham wamejiweka katika nafasi nzuri ya kumsajili kwa mkopo beki wa kati wa Arsenal Carl Jenkinson.

No comments:

Post a Comment