Monday, July 28, 2014

RASMI: LIVERPOOL YAKAMILISHA USAJILI WA LOVREN.

KLABU ya Liverpool, imefanikiwa kukamilisha usajili wa Dejan Lovren uliowagharimu kitita cha euro milioni 24 na kuwa mchezaji wa tatu wa timu hiyo kusajiliwa kutoka Southampton. Beki huyo wa kati alilalamika mapema Julai baada ya kubainisha Southampton walikataa ofa kama hiyo bila kumhusisha lakini sasa amethibitishwa kuwa mchezaji wa tano kusajiliwa na Liverpool kiangazi hiki. Akihojiwa na mtandao wa Liverpool, Lovren amesema ndoto zake zimetimia kuitumikia klabu hiyo ambayo ina mamilioni ya mashabiki duniani kote. Lovren alibainisha kuwa baada ya kucheza katika Uwanja wa Anfield msimu uliopita alijipa matumaini kuwa siku moja lazima aichezee Liverpool na anashukuru ndoto zake zimetimia haraka. Lovren anaongeza orodha ya wachezaji walioihama Southampton msimu huu akiwemo Rickie Lambert na Adam Lallan ambao nao walijiunga na Liverpool, Luke Shaw aliyejiunga na Manchester United, Calum Chambers aliyejiunga na Arsenal huku Morgna Schneiderlin naye akiwa njiani kuondoka baada ya vilabu vya Tottenham Hotspurs na Arsenal kuonyesha nia ya kumtaka.

No comments:

Post a Comment