Thursday, July 31, 2014

EVERTON YAMCHUKUA LUKAKU MOJA KWA MOJA.

HATIMAYE klabu ya Everton imefanikiwa kumchukua moja kwa moja mshambuliaji Romelu Lukaku kwa kitita cha paundi milioni 28. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji mwenye miaka 21 aliyefunga mabao 16 akiwa Everton kwa mkopo msimu uliopita sasa ataitumikia timu hiyo kwa mkataba wa miaka mitano. Meneja wa Everton Roberto Martinez amesema usajili huo sio muhimu tu kwa msimu huu lakini pia ni siku muhimu katika historia ya klabu hiyo. Lukaku alijiunga Chelsea akitokea Anderlecht kwa paundi milioni 18 mwezi August 2011 lakini aliichezea mechi 15 tu. Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amedai kuwa ameamua kumuuza Lukaku kwasababu mchezaji huyo alikuwa haonyeshi moyo kwa kupambania nafasi yake katika kikosi cha chake.

No comments:

Post a Comment