Friday, July 25, 2014

FIFA YAENDELEA KUIBEBA URUSI KUANDAA KOMBE LA DUNIA 2018.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA bado limeendelea na dhamira yake ya Urusi kuandaa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 na kusema kuwa mgomo sio nia sahihi za kupunguza mvutano katika ukanda huo. Mgogoro uliopo kati ya waasi wanaotaka kujiunga na Urusi na serikali ya Ukraine uliangazwa duniani kote wiki iliyopita baada ya kuitungua ndege ya abiria ya Malaysia na kuuwa watu wote 298 waliokuwemo. Moscow wamekuwa wakikanusha kuwasaidia waasi hao lakini kufuatia maafa hayo wabunge waandamizi nchini Ujerumani wamependekeza Urusi kunyang’anywa haki ya kuandaa michuano hiyo. Katika taarifa ya FIFA iliyotumwa katika mtandao wake imedai kuwa bado inachukulia jukumu la kusimamia masuala ya soka kwa makini na wanaunga mkono midahalo yoyote ya amani na kidemokrasia. Taarifa hiyo iliendelea kudai kuwa pamoja na kwamba FIFA haipendezwi na masuala yoyote ya vurugu au uvunjifu wa amani lakini wanajua hawawezi kila migogoro kuitafutia ufumbuzi hususani ile inayohusiana na masuala ya kisiasa. Hivyo FIFA bado itaendelea kuitambua Urusi kama mwenyeji wa michuano hiyo itakayofanyika katikam kipindi cha miaka minne ijayo.


No comments:

Post a Comment