Friday, July 25, 2014

RANIERI ATEULIWA KUWA KOCHA WA UGIRIKI.

CHAMA cha Soka cha Ugiriki-HFF kimethibitisha kumuajiri Claudio Ranieri kama kocha wao mpya wa timu ya taifa. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 62 amesaini mkataba wa miaka miwili akichukua nafasi ya Fernando Santos aliyekiongoza kikosi cha timu hiyo katika michuano ya Kombe la Dunia mpaka hatua ya mtoano alipongolewa na Costa Rica kwa changamoto ya mikwaju ya penati. Ranieri ambaye aliiwezesha klabu ya Monaco ambayo ilikuwa imepanda daraja katika Ligi Kuu nchini Ufaransa kumaliza katika nafasi ya pili msimu uliopita lakini amekuwa akishukutumiwa vikali hatua mabayo imepelekea kuangalia nafasi nyingine. Kibarua cha kwanza cha Ranieri akiifundisha Ugiriki itakuwa ni kuhakikisha wanaanza vyema mechi zao za kufuzu michuano ya Ulaya mwaka 2016, ambapo Septemba 7 mwaka huu watakwaana na Romania. Ugiriki ambao walinyakuwa taji la michuano hiyo miaka 10 iliyopita pia watachuana na Hungary, Finland, Ireland Kaskazini na Visiwa vya Faroe katika kundi F walilopangwa.

No comments:

Post a Comment