Friday, July 25, 2014

MOURINHO AKIRI KUFIKIRIA KUMSAJILI DROGBA.

MENEJA wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho amethibitisha kuwa anafikiria kumsajili tena Didier Drogba. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast aliichezea timu hiyo kwa kipindi cha miaka nane kabla ya kuondoka mwaka 2012 baada ya kuiwezesha Chelsea kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya lakini sasa yuko huru baada ya kuamua kuondoka Galatasaray. Mourinho amesema, Drogba mwenye umri wa miaka 36 bado anaweza mikikimikiki ya Ligi Kuu pamoja na umri alionao ndio maana anafikiria kumrejesha tena Stamford Bridge. Mourinho aliendelea kudai kuwa hafikirii kumsajili kwasababu ya jina lake au kufunga mabao muhimu katika historia ya klabu hiyo au kwasababu anahitaji msaidizi bali ni uwezo wake ambao unaweza kuifanya timu kuwa imara.

No comments:

Post a Comment