Friday, July 25, 2014

OZIL, PODOLSKI, MARTESACKER KUKOSA MECHI YA UFUNGUZI WA LIGI YA ARSENAL.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amebainisha kuwa nyota wake walioshinda Kombe la Dunia wanaweza kukosa mechi ya ufunguzi wa Ligi Kuu nchini Uingereza dhidi ya Crystal Palace. Nyota hao ambao ni Mesut Ozil, Per Martesacker na Lukas Podolski wote wamepewa likizo baada ya kuisaidia Ujerumani kushinda taji la michuano hiyo iliyomalizika hivi karibuni nchini Brazil. Wachezaji hao wanatarajiwa kurejea mazoezini ya maandalizi ya msimu Agosti 11 ikiwa ni siku tano kabla ya mchezo huo dhidi ya Palace. Wenger amesema amewapa wachezaji hao likizo ndefu kidogo kwasababu ana uzoefu na wachezaji waliocheza fainali za Kombe la Dunia kwamba wanahitaji muda wa kupumzika. Kocha huyo aliongeza kuwa anajua wanaweza kujiandaa vizuri lakini kwa ajili ya mchezo wa kwanza utakaochezwa Agosti 16 hadhani kama watakuwa tayari.

No comments:

Post a Comment